Thursday, 17 July 2014

DEMBA BA AELEKEA UTURUKI


Aliyekua Strika wa Chelsea Demba Ba


  Aliyekua Strika wa Chelsea Demba Ba amewasili Uturuki anakotarajiwa kukamilisha uhamiaji wake kutoka Chelsea hadi Besiktas kwa gharama ya £8m. Strika huyo mwenye umri wa mika 29 ameyathibitisha hayo katika mtandao wa Twitter akiwaamevalia  jezi ya Besi-ktas.Aidha.Wakati uo huo Chelsea wamejibu kwa kumshawishi Filipe Luis aihame Atletico Madrid ili ajiunge nao.Msimu uliopita Luis alishiriki mechi zaidi ya 40 na kilele ikawa Atletico kushinda La Liga kwa mara ya kwanza tangu 1996.Demba Ba amewahi kuifungia Chelsea mabao 14.

Said PiePie,Nairobi.

ARSENALI YAPANIA KUMNASA KHEDIRA


Sami Khedira aliyekua kiungo wa Real Madrid

    Klabu ya Arsenali imefikia hatua ya kumsajili kiungo wa kati  Sami Khedira.tokea Real Madrid kwa kima cha £20m.Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 ni mzawa wa Tunisia laikini kwa sasa anasakata soka ya kulipwa nchini Ujerumani kandarasi yake bado ipo kule  Santiago hadi mwaka wa 2015.Maelewana na klabu ya Arsenali wanazidi kunoga,aidha wanabunduki wamesha wasajili mhispania Alexis Sanchez ambaye hapo awali alikua akiwasakatia Barcelona.


 Said PiePie,Nairobi.

DIEGO AELEKEA CHELSEA


Diego Costa aliyekua strika wa  Atletico Madrid,
Strika wa Atletico Madrid,Diego Costa amejiunga na klabu ya Chelsea kwa kwa kandarasi ya miaka mitano kwa kima cha  £32mAidha mshambulizi huyo amekuwa mchezaji wa tatu kujiunga na Chelsea baada ya Cesc Fabregas na Mario Pasalic.Costa amefungia Atletico mabao 52  msimu uliopita ambapo walishinda taji la kwanza la La Liga tangu 1996 na kufikia kuwa mabingwa wa ligi.Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho aliongeza mshambulizi matata katika kipindi hicho.Costa atajiunga na mchezaji mwenza wa kimataifa Cesc Fabregas kutokana na matokeo duni ya uhispania katika kombe la dunia ambapo walibanduliwa nje katika hatua ya kwanza ya kikundi.Wakati uo huo Costa ameonyesha furaha yake kujiunga na Chelsea akisema kuwa ataonyesha umahiri wake ulaya.

Said PiePie,Nairobi.

Wednesday, 16 July 2014

GAAL AWASILI OLD TRAFORD LEO


Louis van Gaal kocha wa Manchester United
    Louis van Gaal anaingia hii leo Old Trafford  na kuannza rasmi kuwanoa Manchester United.
Aidha Meulensteen aliyefanya kazi na  Sir Alex Ferguson hapo awali amekiri kuwa itamchukuaLouis van Gaal ngavi ngumu kukiivisha kikosi cha United ambacho kimzembea kwa sasaMechi yao ya kwanza msimu ujao United watafungua pazia na klabu ya  Swansea.Man United walimaliza msimu uliopita katika nafasi ya saba jambo ambalo liliwaudhi maafisa wa klabu hiyo pamoja na mashabiki wa United dunia nzima.Hali iliyochangia kutimuliwa kwa david Moyes.Gaal aliwaongoza Uholazi kufika michuano ya semi fainali kombe la dunia nchini Brazil mwaka huu.

Said PiePie,Nairobi.

LIVERPOOL YAMSAJILI MARKOVIC


Lazar Markovic aliyekua mchezaji wa Benfica
 Klabu ya  Liverpool imemsajili  Lazar Markovic  kwa kima cha Pauni millioni 20 kutoka Benfica.Mserbia huyo aliiwezesha klabu ya Benfica kutwaa taji la Ureno msimu uliopita na anasema anamatumaini makubwa ya kuwaridhisha mashabiki na mwenye club hiyo.Katika dirisha la usajili msimu huu Liverpool wamenasa wachezaji kadhaa wakiwemo Mshambuliaji Rickie Lambert, 32 kwa pauni £4m na Adam Lallana, mwenye umri wa miaka 26, kwa pauni £25m, wote walitokea Southampton na Divorc Origi kutokea humu nchini.

Said PiePie,Nairobi.

Tuesday, 15 July 2014

VIJANA WA TRANZOIA WAREJEA KUTOKA BRAZIL

   
Baadhi ya vijana wanao sakatia Trans Nzoia Youth Sports Association,

  Timu nchini wa umri usiozidi  miaka 18 ya Trans Nzoia Youth Sports Association,, kutoka nchini Kenya wamerejea nyumbani baada ya kushiriki kwenye mashindano ya wachezaji watano kila upande ya Football For Hope Festival mjini Rio De Janeiro, Brazil.Timu ya Delta Culture ya Cape Verde ilishinda mashindano hayo kwa kuilaza Sport Dans La Ville ya Ufaransa bao 1-0 mechi ya fainali.Timu  ya Cape Verde na Tysa ni baadhi ya timu nane za Afrika zilizoshiriki mashindano hayo yaliyojumuisha timu kutoka mataifa 32.Wachezaji hao, walitizama mechi ya robo-fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa wanasema mbali na kandanda, wamejifunza mengi kuhusu maadili mema.Timu hiyo ilimaliza mechi zake zote bila kupoteza.

Said PiePie,Nairobi.

STARS KUMENYANA NA BURUNDI LEO


Kikosi cha Stars katika kambi ya mafunzo
      Timu ya taifa ya harambee stars itachuana na Burundi katika mechi ya kirafiki hii katika uga wa Nyayo.Mechi ya leo ni katika maandalizi ya michuano ya  kufuzu  AFCON 2015 mechi itakayo karagazwa huku Lesotho katika uga wa Maseru Julai 20.
Katika mchuano wa leo refarii wa katikati ya uwanja ni Ssali Mashood akisaidiwa na Bugembe Hussein na   Ngobi Balikoowa wote kutokkea nchi ya Uganda.Mechi hiyo imeratibiwa kusakatwa hii leo saa kumi na moja jioni katika uga wa Nyayo

Said PiePie,Nairobi.

Monday, 14 July 2014

SCHOLARI APIGWA KALAMU


  Luis Felipe Scolari,aliyekua kocha wa Brazil
   S
hirikisho la kandanda nchini brazil limempiga kalamu kocha ya timu ya taifa hilo Luis Felipe Scolari baada ya kuandikisha matokeo duni katika kombe la dunia lililomalizika hapo jana.Brazil walizabwa 3-0 na Uholanzi  siku ya Jumamosi,hata hivyo habari rasmi itatolewa baadaye hii leo. Aidha Delfim Peixoto, mmoja wa wanalkamati wa shirikisho hilo amesema kuwa Scholkari hatasalia kuwa kocha wa timu hiyo baada ya kuonyesha mchezo duni.Scholari iliongoza Brazil mwaka wa 2002 katika michuano ya kombe la  dunia nchini Japa.Habari hizi zime chapishwa na Globo TV

Said PiePie,Nairobi.

UJERUMANI BINGWA WA KOMBE LA DUNIA 2014



Ujerumani watawazwa mabingwa wa kombe duina 2014 nchini Brazil
            Shangwe,nderemo,vifijo ziligubika anga ya uga wa Estadio Mineirao mjini Rio de Janeiro Brazil jana baada ya Vijana wa Joachim LoewUjerumani kuwalaza 1-0 Argentina na kutawazwa mabingwa wa kombe la dunia 2014.Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Loew  amesema ndoto ya timu kutwaa kombe la dunia ilitimia hapo  jana usiku. Mchezaji kiungo Mario Goetze-Super Mario aliingia kwenye madaftari ya  vya historia pale alipopachika goli la ushindi katika fainali za kombe la dunia, lililoipatia Ujerumani ubingwa wa dunia. Nyota huyo wa klabu ya Bayern Munich alitegua kitendawili cha ubingwa katika dakika  za nyoneza (113)  na kuinyamanzisha Argentina, huku ndoto ya Lionel Messi ya kufuata nyayo za nguli Diego Maradona ikiishia kwa kushindwa.
Ujerumani sasa imeshinda kombe la dunia mara nne, na kulifanya taifa hilo kubwa duniani kuwa nyuma tu ya Brazil yenye rekodi ya ushindi mara tano. Muda wa maamuzi wa fainali hiyo iliyojawa na msisimko na magoli yaliyofungwa kwa ustadi mkubwa ulikuja wakati timu hizo zikinyemelewa na mikwaju ya penati mbele ya watazamaji 74,738 katika uwanja maarufu wa Maracana mjini Rio de Janeiro.Mchezaji bora wa mechi hiyo ya fainali Goetze aliituliza kifuani krosi ya Andre Schuerrle na bila kufanya ajizi akasukuma mkwaju uliyomduwaza mlinda mlango wa Argentina Sergio Romero, kwa goli la ushindi lililomfanya nahodha Philip Lahm kubeba kombe la dunia.





 
Mario Gotze aadhimisha bao lak
Ujerumani ambayo iliinyeshea Brazil mvua ya magoli 7 -1 katika mchezo wa nusu fainali, imekuwa timu ya kwanza ya Ulaya kubeba kombe la dunia katika Amerika ya Kusini. Walianza kushinda taji hilo mwaka 1954, na kulirudia mwaka 1974 na 1990. Wamekuwa wakilikosakosa ama kwa kutolewa kwenye hatua ya nusu fainali au fainali katika miaka ya hivi karibuni.Lionel Messi hakucheza kama alivyotarajiwa. Kiungo wa kati Javier Mascherano alisema ni vigumu kueleza, kwani walifanya kila kitu kushinda na walikuwa na nafasi nzuri zaidi.Aidha Messi, Gonzalo Higuain na Rodrigo Palacio walikosa nafasi nzuri cha juu wakati kichwa cha Benedikt Hoewedes kiligonga mwamba kwa upande wa Ujerumani mbele ya maelfu ya mashabiki wakiwemo rais wa Ujerumani Joachim Gauck, Kansela Angela Merkel, rais wa Urusi Vladmir Putin na mwenyeji wao rais wa Brazil Dilma Roussef.




 
Mbwembwe za mashabiki wa Ujerumani
Wakiwa wamebeba kombe mikononi mwao, wachezaji wa Ujerumani waliimba pamoja na mashabiki wao, wimbo maarufu wa Am Tag Wie Diesen (Katika siku kama hii) uliyopigwa na bendi ya Ujerumani ya Die Toten Hosen na kuchezwa uwanjani. Ilikuwa ndoto iliyotimia baada ya subira ya miaka mingi.Kufuatia ushindi huo Ujerumani walinyakua taji la nne la dunia.Kipa wa Ujerumani Manuel Nuer alitawazwa kuwa kipa bora na akatuzwa ''Golden Glove''.Rais wa Urusi Vlamir Putin alipokea ithibati rasmi ya kuandaa makala yajayo ya kombe la dunia kutoka kwa rais wa FIFA.Rais wa Urusi Vladimir Putin alikuwepo Maracana kwa mualiko wa rais wa FIFA Sepp Blatter na rais wa Brazil Dilma Rousseff. Makala yajayo ya kombe la dunia yataandaliwa nchini Urusi mwaka wa 2018.



Said PiePie,Nairobi.

Saturday, 12 July 2014

GOR YAZIMA STIMA


Kikosi cha Gor kwenye mbwembwe
     Gor Mahia imeandikisha ushindi mnono hii leo baada ya kuwalaza Western Stima  2-0 katika mchuano wa ligi ya primia nchini ulio karagaziwa katika uga wa Afraha mjini Naivasha jioni ya leo. Eric Ochieng aliyekuwa mchezaji wa  Talanta FC hapo awali na Timothy Otieno waliwatia Kogalo kifua mbele kwa kufunga mabao mawili mtawalia.Gor walimiliki mpira kwa mda mrefu katika dakika za kwanza hata hivyo katika dakika ya nane Stima walivamia lango la Gor huku wakiponea kwenye tundu la sindano.
Baadhi ya wachezaji wa Western Stima
Bao la kwanza la Gor lilipatikana katika dakika ya 61 kupitia kona iliyocharazwa na   Erick Ochieng.Huku bao la pili likitiwa kimiani naTimothy Otieno.












  Aidha kocha wa Gor,Bobby Williamson amewapongeza vijana wake kwa kuonyesha mchezo mzuri uliokomaa.Refarii wa katikati ya uwanja alikua  Amos Ichingwa.Wakati uo huo Sony sugar iewalaza Tusker Fc 1-0


Said PiePie,Nairobi.

USALAMA WAIMARISHWA RIO DE JENEIRO



         
     Maafisa wa polisi  mjini Rio de Jeneiro wameanza kuweka usalama na ulinzi mkali huku masaa yakihesabuliwa fainali za kombe la dunia zing'oe nanga hapo kesho kati ya Argentina na Ujerumani Zaidi ya maafisa elfu hamsini wa polisi,maafisa wa zima moto,pamoja na majeshi yatashirikishwa katika kuimarisha ulinziRais wa Brazil Dilma Roussef anatarajiwa kuhudhuria fainali hizo katika uwanja wa Maracana akiandamana na marais wengine tisa akiwemo rais Vladmir Putin wa Urusi na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani.
Meli ishirini na tano zitakuwa zinapiga doria katika pwani ya mji huo.
Huku hayo yakijiri, Ujerumani inajiandaa kushuka dimbani katika fainali ya Kombe la Dunia katika uwanja wa Maracana Brazil, dhidi ya Argentina huku ikipigiwa upatu kumzidi nguvu mpinzani wake huyo wa Amerika ya Kusini.


Kikosi chaUjerumani katika kambi ya maandalizi
Katika mechi tatu za mwisho ambazo timu hizo zimekutana, Wajerumani ndio walioibuka washindi. Ujerumani ilishinda katika fainali ya 1990 mjini Rome 2-1 na kuwa bwaga Argentina katika robo fainali za Kombe la Dunia 2006 kupitia mikwaju ya penalti  mjini Berlin, na tena ikawachabanga magoli manne kwa sifuri katika robo fainali miaka minne iliyopita mjini Cape Town, Afrika Kusini. Nayo Argentina iliipiku iliyokuwa Ujerumani ya Magharibi magoli matatu kwa mawili katika fainali ya 1986 mjini Mexico City.


Brazil inachuana na Uholanzi hii leo.AidhaLoius Van Gaal, kocha wa Uholanzi anasema mchuano huu huwa hauna maana. Mechi ya kumtafuta mshindi wa tatu kwa kawaida huwa siyo maarufu, na kivumbi cha leo mjini Brasilia kitakuwa tu cha kuwaliwaza wenyeji Brazil ambao bado wana maruweruwe ya kichapo walichopewa na Ujerumani.


 Said PiePie,Nairobi.






Friday, 11 July 2014

SANCHEZ AWASILI EMIRATES


Alexis Sanchez aliyekua mchezaji wa Barcelona hapo awali

      Hatimaye klabu ya Arsenali imenasa huduma za mchezaji Alexis Sanchez kutokea klabu ya Barcelona kwa kima cha dola pauni 32.Sanchez mwenye umri wa miaka 25 ndiye mchezaji wa kwanza kusajiliwa msimu huu aidha Arsenali inapania kunasa Mathieu Debuchy kutoka klabu ya Newcastle.Wakati uo huo Sanchez ameonuesha kuridhika kwake kuhaima klabu ya Arsenali akisema anatarajia kupata tajriba ya juu n klabu hiyo.Klabu hiyo pia anammezea mate kiungo wa kati mzaliwa wa Tunisia anayeisakatia  Ujerumani Sami Khedira hata hivyo duru zinaripoti kuwa  kitita ambacho Khedira huenda akalipwa kitamfanya awe mchezaji ghali katika kambi ya wanabunduki.

Said PiePie,Nairobi.