Strika wa Uruguay Luis Suarez anakabiliwa na marufuku itakayomlazimu kukosa mechi nyengine za michuano ya kombe la dunia
iwapo atapatikana na hatia ya kumng'ata mchezaji wa Italy Giorgio Chiellini katika mechi ya hapo jana.
Shirikisho la soka duniani FIFA
limeanzisha uchunguzi wa kumuadhibu mcheza huyo kufuatia ushindi wa moja kwa
bila dhidi ya Italy.
Chiellini amedai kwamba Suarez
alimng'ata bega lake licha ya Suarez kudai kuwa ni mchazaji huyo aliyemchezea
vibaya.
![]() |
Giorgio Chiellini aonyesha jeraha baada ya kung'atwa na Suarez |
Suarez mwenye umri wa miaka 27 huenda akapigwa marufuku ya kutoshiriki katika mechi 24 ama miaka miwili.
Refa aliyesimamia mechi hiyo kutoka Mexico Marco Rodriguez hakuchukua hatua yoyote kufuatia kisa hicho,lakini FIFA bado inaweza kumuadhibu Suarez.
Aliyekuwa mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya Liverpool Jan Molby anatarajia kwamba Suarez atapigwa marufuku kwa mechi zote za kombe hilo zilizosalia.
Said PiePie,Nairobi.