Rais M’Bolhi golkipa wa Algeria amekanusha madai wachezahi wao walishindwa na Ujerumani kutokana na wao kuwa
wadhaifu kwa kufunga saumu.M’Bolhi ambaye alichaguliwa kuwa
mchezaji bora katika mechi hiyo ambayo Algeria walishindwa mabao 2-1 na
Ujerumani katika muda wa ziada anasisitiza kuwa Saumu hakikuchangia kwao
Kushindwa.Aidha M’Bolhi anasema kuwa wachezaji
hao wamekwisha zoea kucheza hata wakiwa kwenye mfungo na hivyo haipaswi
kutolewa kama sababu .Kabla ya mechi hiyo kulikuwa na
ubishi baada ya kocha wa Algeria Vahid Halilhodzic kukataa kuulizwa maswali kuhusiana
na mfungo wa Ramadhan ambao ulikuwa umeanza jumamosi .Halilhodzic alikataa kufichua idadi
ya wachezaji wake ambao wanafunga mfungo wa Ramadhan kabla ya mechi .Wakati uo huo kocha huyo alikataa kujibu swali ikiwa wachezaji wake watafunga Ramadhan au la wakati
wakicheza.Kulingana na dini ya Kislamu ,Ramadhan ni nguzo muhimu ya dini na ifikapo wakati huo kila mtu
mwenye umri wa baleghe hujinyima chakula kuanzia alfajiri hadi magharibi .Hiyo inaamisha kuwa wachezaji wa
Algeria hawakuwa wamekula chochote hadi baada ya kipindi cha pili cha mechi
hiyo ndipo waliporuhusiwa kunywa na kula .Ujerumani
ilifuzu kwa robo fainali ya kombe la dunia ambapo watakutana na Ufaransa ijumaa
ijayo.
Said PiePie,Nairobi.
No comments:
Post a Comment