Klabu za ligi kuu ya soka nchini England zimeafikiana kutumia teknolojia ya camera katika maamuzi ya mchezo wa soka 
kuanzia msimu ujao.
Kampuni ya Uingereza ya Hawk-Eye imepewa mkataba wa kufunga vifaa maalumu kwenye viwanja vyote 20 
vya timu za ligi kuu nchini England.
Hawk-Eye inajulikana kwa 
 teknolojia kama hiyo kwenye mchezo wa Tenesi na Kriketi,ambapo camera 
maalumu huweza kutambua iwapo mpira umegusa mstari ama la na kumjulisha 
mwamuzi na wasaidizi wake ndani ya sekunde chache.
Chama cha soka nchini England FA,kitafunga vifaa
 hivyo kwenye uwanja wa Wembley tayari kwa kutumika kwenye mchezo wa 
ngao ya jamii hapo mwezi wa nane mwaka huu.
Viwanja vya timu 17 zitakazosalia ligi kuu na
 zile 3 zitakazopanda daraja vitawekewa teknolojia hiyo na shughuli 
nzima itachukua wiki sita kukamilika.Msukumo wa kutumia teknolojia maalumu ya 
kutambua goli ilipata nguvu baada England kukataliwa goli lao la 
kusawazisha walipocheza na Ukraine,Mchezo ambao England walifungwa bao 
moja kwa bila kwenye michuano ya kombe la mataifa barani Ulaya mwaka 
2012, Ambapo mwezi mmoja baadaye bodi ya vyama vya soka vya kimataifa 
(IFAB) katika kikao chake mjini Zurich kilipitisha teknolojia mbili ili 
zitumike kwenye michezo ya soka.Rais wa FIFA 
Sepp Blater amesema kukataliwa kwa goli la Frank 
Lampard kwenye mechi ya robo fainali kati ya England na Ujerumani mwaka 
2010 katika michuano ya kombe la dunia,kulichangia kwa kiasi kikubwa 
maamuzi ya shirikisho hilo kupitisha sheria ya matumizi ya teknolojia ya
 kutambua goli.
Chama cha soka cha England kimesema teknolojia hiyo itaaanza kutumika msimu ujao.Kwa sasa Goal  Technology inatumika katika michuano ya kombe la dunia nchini Brazil.
Said PiePie,Nairobi.