Monday, 16 June 2014

GOR YAMSAINI OTIENO




       
 
Timothy Otieno Talanta Fc

     Klabu ya Gor mahia ametia mkataba wa miezi sita na kiungo wa kati  wa Talanta FC Timothy Otieno,Kiungo huyo anauwezo mkubwa na aliisaidia klabu yake hapo awali kunyakua mataji kadhaa hatua iliyopelekea klabu nyingi kummezea mate. Kiungo huyo.Alifuzu kutoka National Youth Talent Academy (NYTA) pia ni mwanafunzi wa zamani wa shule ya upili ya Kakamega.

Said PiePie,Nairobi.

GOAL TECHNOLOGY KUTUMIKA EPL MSIMU UJAO








         Klabu za ligi kuu ya soka nchini England zimeafikiana kutumia teknolojia ya camera katika maamuzi ya mchezo wa soka kuanzia msimu ujao.
Kampuni ya Uingereza ya Hawk-Eye imepewa mkataba wa kufunga vifaa maalumu kwenye viwanja vyote 20 vya timu za ligi kuu nchini England.
Hawk-Eye inajulikana kwa  teknolojia kama hiyo kwenye mchezo wa Tenesi na Kriketi,ambapo camera maalumu huweza kutambua iwapo mpira umegusa mstari ama la na kumjulisha mwamuzi na wasaidizi wake ndani ya sekunde chache.
Chama cha soka nchini England FA,kitafunga vifaa hivyo kwenye uwanja wa Wembley tayari kwa kutumika kwenye mchezo wa ngao ya jamii hapo mwezi wa nane mwaka huu.
Viwanja vya timu 17 zitakazosalia ligi kuu na zile 3 zitakazopanda daraja vitawekewa teknolojia hiyo na shughuli nzima itachukua wiki sita kukamilika.Msukumo wa kutumia teknolojia maalumu ya kutambua goli ilipata nguvu baada England kukataliwa goli lao la kusawazisha walipocheza na Ukraine,Mchezo ambao England walifungwa bao moja kwa bila kwenye michuano ya kombe la mataifa barani Ulaya mwaka 2012, Ambapo mwezi mmoja baadaye bodi ya vyama vya soka vya kimataifa (IFAB) katika kikao chake mjini Zurich kilipitisha teknolojia mbili ili zitumike kwenye michezo ya soka.Rais wa FIFA Sepp Blater amesema kukataliwa kwa goli la Frank Lampard kwenye mechi ya robo fainali kati ya England na Ujerumani mwaka 2010 katika michuano ya kombe la dunia,kulichangia kwa kiasi kikubwa maamuzi ya shirikisho hilo kupitisha sheria ya matumizi ya teknolojia ya kutambua goli.
Chama cha soka cha England kimesema teknolojia hiyo itaaanza kutumika msimu ujao.Kwa sasa Goal  Technology inatumika katika michuano ya kombe la dunia nchini Brazil.

Said PiePie,Nairobi.

TUSKER YAZIDI KUNOGA



Tusker  Fc washerehekea ushindi wao dhidi ya Ingwe
     Nahodha wa  Tusker Fc  almaarufu wanamvinyo Samwel Odhiambo amesema kuwa timu yake iko katika hali nzuri yaku kung’ang’ania taji la KPL msimu huu alisema haya mapema hii leo.Hapo jana Wanamvinyo hao ilicharaza Inmgwe mabao 2-1 katika mechi za Nane bora katika  uchanjaa wa Kinoru,Meru.Kwa sasa Tusker inashikilia nafasi ya tatu na alama 27 katika jedwali la ligi ya primia humu nchini.



Said PiePie,Nairobi.