![]() |
Kikosi cha Brazil kikinoa makali |
Thiago alionyeshwa kadi yake ya pili timu hiyo ilipoilaza Colombia Ijumaa iliyopita.
wakati uo huo Brazil wamepata pigo kwani Mshambuli machachari Neymar ambaye alijeruhiwa uti wa mgongo.Kocha wa Brazil Scolari anapanga kutumia Willian kuziba pengo la Neymar.Scolari amesema kuwa Brazil itajitahidi dhidi ya Ujerumani licha ya kumkosa Neymar ambaye alikuwa ameifungia mabao manne.Aidha kocha wa Ujerumani Joachim Low amesema kuwa Samba boys ni wakakamavu na wana jituma katika safu zao mbalimbali.
![]() |
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Ujerumani |
Low amemtaka refarii wa Mexico Marco Antonio Rodriguez kutolegeza kamba dhidi ya wenyeji hao kutokana na nyendo zao .Timu hizo zitafungua kampeini yao katika mechi ya kwanza ya nusu fainali huko Belo Horizonte.Matumaini ya wenyeji kutwaa ubingwa wa dunia yameimarika baada ya timu hiyo kufuzu kwa nusu fainali .
Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana Brazil iliwalaza Ujerumani 2-0 mwaka wa 2002 katika kombe la dunia huko Japan.Ujerumani Ilifuzu kwa nusu fainali hiyo baada ya kusajili ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ufaransa katika mechi ya robo fainali.Mechi kati ya Brazil na Ujerumani iitakaragazwa hii leo mwendo wa saa tano usiku katika uga wa Mineirao jijini Belo Horizonte
Said PiePie,Nairobi.