Thursday, 26 June 2014

SUAREZ NJE MIEZI 4

Luiz Suarez strika wa Uruguay
    Luis Suarez amepigwa marufuku ya mechi tisa na shirikisho FIFA baada ya kupatikana na kosa la kumng'ta Giorgio Chiellini kwenye mechi yao ya kombe la dunia nchni Brazil.Suarez pia  hatajihusisha na shughuli za kandanda kwa miezi minne na kutozwa faini ya dola elfu mia moja.Kutokana na adhabu hiyo Suarez sasa hatashiriki tena kwenye mechi zilizosalia za kombe la dunia.Kutokana na adhabu hiyo iliyochukuliwa na kamati ya nidhamu ya Fifa Suarez sasa hatashiriki kwenye mechi ya raundi ya pili kati ya Uruguay na Columbia Juni tarehe 28.
Adhabu hiyo pia inamaanisha Suarez hatashiriki kwenye mechi za Uruguay zijazo za kombe la dunia endapo timu itazidi kusonga mbele na zile zijazo za kufuzu kwa mashindano ya kombe la dunia.
Kamati hiyo ya nidhamu ya Fifa imesema Suarez hatakiwi kuingia kwenye uwanja wowote Uruguay inapocheza wakati wa adhabu hiyo ya kutocheza mechi tisa za kimataifa.Ripoti hii imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya Fifa Claudio Sulser .Aidha Kamati ya Fifa imetilia maanani kila kitu kwenye kitendo hicho kabla ya uamuzi huo.Mashabiki wengi duniani wamemshutumu vikali Suarez kwa kumng'ata mchezaji huyo wa Italia kwani hii ni mara ya tatu anapatikana na hatia hiyo.

Said PiePie,Nairobi.

UFARANZA KUKUTANA NA NIGERIA MKONDO WA PILI



Kikosi cha timu ya Ufarnza
         Ufaranza ilikamilisha mechi za makundi kwa sare tasa dhidi ya Ecuador.Kwa sasa Ufaransa imesalia kileleni mwa kundi E ikiwa na alama 7 moja zaidi ya Switzerland iliyoisakama Iran katika mechi ya mwisho.Nao Argentina  walifuzu katika raundi ya 16 bora ambapo sasa watachuana na Nigeria .Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Mechi hiyo ilishuhudia kadi nyekundu ya nane katika mashindano haya ya kombe la dunia ,nahodha wa Ecuador Antonio Valencia alipofurushwa uwanjani baada ya kumchezea vibaya Lucas Digne.Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Ufaransa sasa itamenyana  na Nigeria waliomaliza mechi yao ya kundi F kwa kushindwa na Argentina kwa mabao 3-2 siku ya Jumatatu tarehe 30 katika Estadio Di Nationale.Washindi wa kundi hilo Argentina watakuwa na kibarua kigumu dhidi ya Switzerland Jumanne ijayo katika uga wa Arena De Sao Paulo.


 Said PiePie,Nairobi.

FIFA YAMPIGA MARUFUKU BECKNERBAUER



 
Aliyekua Kocha wa Ujerumani Franz Beckenbauer

           Franz Beckenbauer amepigwa marufuku ya siku 90 kujihusisha na soka kwa kushindwa kutoa ushikiano wake kwa kamati ya uchunguzi ya FIFA.
Aidha FIFA imedokeza kuwa Beckenbauer alikua katika  kamati kuu ya Shirikisho la Kimataifa la soka (FIFA) ambalo mwaka 2010 li iliwapatia Qatar kuandaa michuano ya michuano  ya Kombe la Dunia kwa mwaka 2022,aliombwa mara kadhaa kutoa maelezo yake kuhusu uamuzi huo tata.Marufuku hiyo imewekwa kufuatia ombi la mwanasheria wa Marekani Michael Garcia mkuu wa jopo la uchunguzi wa kamati ya maadili ya FIFA ambaye anaongoza uchunguzi kuhusu uamuzi huo wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022.
         Jumatano Garcia aliuambia mkutano mkuu wa FIFA wa kila mwaka mjini Sau Paulo Brazil kwamba yeye na kamati yake tayari walikuwa na sehemu kubwa ya mamilioni ya nyaraka ambazo zimetajwa na gazeti la Sunday Times la Uingereza katika repoti ya karibuni inayodai kutolewa kwa rushwa katika harakati za kufanikisha Qatar ipate nafasi ya kuandaa michuano hiyo ya soka Kombe la Dunia.
Gazeti la Sunday Times limesema baadhi ya mamilioni ya nyaraka imeziona kuwa zinahusiana na malipo yaliyotolewa na mjumbe wa zamani wa kamati kuu ya FIFA Bin Hammam kwa maafisa ikiwa kama sehemu ya kampeni ya kuungwa mkono kwa harakati za Qatar kuandaa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
Kesi hiyo hivi sasa iko kwenye taratibu rasmi za uchunguzi chini ya mjumbe wa jopo hilo Vanessa Allard akiwa kama mkuu wa uchunguzi.Repoti rasmi ya uchunguzi huo inatarajiwa kutolewa hapo mwezi wa Julai.

Said PiePie,Nairobi.