Thursday, 12 June 2014

WACHEZAJI KADHAA KUKOSA MECHI ZA LIGI YA PREMIA






    Wachezaji watatu wa ligi ya primia watatakosa mechi katika  juma la 15 baada ya kuonyeshwa kadi za njano.Timu ya SoNy Sugar itakosa hudumu za Edwin Oduor  baada ya kupata kadi 5 za manjano wakati  wa mechi kati yao na Muhoroni katika Uga wa Awendo mnamo Juni 15,huku wanamanasi Thika United watakosa huduma za mlindalango Dennis Odhiambo wakati wa mchuano wao na Mathare United katika uga wa Nyayo siku ya City Stadium.Odhiambo anakadi 5 za manjano.

Said PiePie,Nairobi

INGWE YAFUZU FAINALI ZA NANE BORA






 

      Timu ya AFC Leopards hapo jana ilinyakua ushindi baada ya kuwalaza kcb 3-0 katika mchuano wa timu nane bora katika mechi ya nusu fainali.Austin Ikenna ,Jacob Keli  and Bernard Mang’oli  waliisaidia Leopards kunyakua ushindi huo. Wanabenki KCB walionyesha mchezo mzuri katika kipindi cha kwanza hata hivyo walikumbwa na utasa wa mabao.KCB walifanya badiliko katika dakika za kwanza za 12 baada ya kiungo wao wa kati Hedson Mauda kujeruhiwa pengo  lake lilijazwa na Ronald Musana aliyesajiliwa majuzi
          Mabeki ya KCB walizembea mnamo dakika ya 40 nakumpa  fursa Paul Were aliipenyeza pasi ya kimanjaro kwake Bernard Mangoli wingi wa kushoto naye hakusita ila alimpeleka madukani mlinda lango wa KCB Caleb Wafula huku akiiandikia Ingwe bao la pili
Kipindi cha pili kilianza na mabadiliko huku Joseph Shikokoti akitolewa nje na nafasi yake ikimilikiwa na  Eric Masika.Kwa sasa ingwe imejikatia tiketi ya fainali itakapo kutana na wanamvinyo Tusker FC Juni 15.

Said PiePie, Nairobi

KOMBE LA DUNIA BRAZIL 2014






    Rais wa Brazil Dilma Rousseff amewaomba  wananchi nchini humo kuungana pamoja kwa ajili ya Kombe la Dunia la 2014, akisema taifa liko tayari licha ya Migomo na maandamano ambayo yameshuhudiwa nchini humo.Katika hotuba yake iliyorushwa kwenye televisheni kabla ya ufunguzi wa tamasha hilo, rais huyo amesema macho ya ulimwengu mzima yanaiangazia Brazil akisema nchi hiyo ilikabiliana na changamoto kubwa na sasa iko tayari ndani na nje ya viwanja kwa ajili ya burudani hilo la soka.
Huku hayo yakijiri vitisho vilivyokuwepo vya  mgomo vimeondolewa kwa muda huku wafanyakazi wa treni za chini ya ardhi mjini Rio wakiufutilia mbali mgomo wao baada ya kupewa nyongeza ya mshahara ya asilimia 8. Mgomo wa siku tano wa usafiri mjini Sao Paulo pia ulisitishwa Jumatatu wiki hii, ijapokuwa huenda ukarejea tena wakati michuano itakapoanza kama wafanyakazi waliopigwa kalamu hawatorudishwa kazini.
     Sherehe za ufunguzi wa dimba hilo zinaandaliwa katika uwanja wa Corinthians Arena, mjini Sao Paulo hii leo, miongoni mwa wageni watakaohudhuria ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon pamoja na viongozi 12 wa nchi na serikali.
Baada ya sherehe za ufunguzi, vijana wa kocha Luiz Felipe Scolari, watashuka dimbani kupambana na Croatia katika mechi ya ufunguzi ya Kundi A. Na kama wenyeji hao wataweza kufika katika fainali na kunyakua taji hilo mnamo Julai 13, watakuwa timu ya tatu pekee iliyocheza mechi ya ufunguzi kuwahi kufanya hivyo.
Katika michuano 19 ya Kombe la Dunia,  Italia pekee  mwaka wa 1934 na England mwaka wa 1966 zilizowahi kucheza mechi ya kwanza na  kushinda katika fainali. Zaidi ya wanajeshi na polisi 150,000 watashika doria k wakati wa dimba hilo.

Said PiePie,Nairobi