Monday, 30 June 2014

INGWE HAIKOPESHI KWA SASA.



Kikosi cha Leopards alamaarufu Ingwe

             Timu ya AFC Leopards imefutilia mbali uhamisho wa wachezaji wake iliokuwa imepania kuwasajili kwa mkopo,miongoni mwa wachezaji hao ni pamoja na Strika Dennis Dodi, Duncan Otieno na Sadiq Mohammed.Kulingana na katibu wa Ingwe Timothy Lilumbi amesema kuwa maelewano na klabu mbalimbali hayajaafikiwa.Leopards ilikua inapania kusajili wachezaji katika klabu ya Kakamega Homeboyz, Thika United na Mathare United.


Said PiePie,Nairobi.

PODOSKI KUKOSA MECHI DHIDI YA ALJERIA



Lukas Podolski Strika wa Ujerumani
     Lukas Podolski hatashiriki  mchuano wa kufuzu katika robo fainali dhidi ya Algeria utakaochezwa hii leo.Kocha wa Ujerumani Joachim Löw amewadokezea waandishi habari katika kambi ya mafunzo ya Ujerumani ya Santo Andre kuwa Podolski hatakuwa tayari kwa wakati unaofaa kucheza mpambano wa Algeria, akisema kuwa mchezaji huyo wa pembeni wa Arsenal atastahili kupumzika kwa siku mbili au tatu.Beki Jerome Boateng amepata jeraha jingine, mara hii akiumia katika goti lake la kushoto. Löw amesema jeraha hilo siyo ba ya sana.Dhidi ya Algeria, Ujerumani inapambana na timu dhabiti zaidi ya Afrika katika dimba hilo kufikia sasa. Löw amesema Desert Warriors ni hatari mno na wenye nguvu uwanjani na hivyo haitakuwa kazi rahisi kwa vijana wake, hata hivyo  ameongeza kuwa timu yake inaweza kuimarika baada ya kutoka sare na Ghana na kuwapiku kwa ushindi mdogo sana timu ya Marekani yake Jürgen Klinsmann katika hatua ya makundi.

Said PiePie,Nairobi


"SIKUANGUSHWA" ROBBEN AKIRI.


Strika wa Uholanzi Arjen Robben katika mechi dhidi ya Mexico
                    Strika wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa hakutegwa bali alijiangusha tukio lilisababisha tim uyake kutuzwa penaltiWakati uo huo kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .Robben alikunguwa katika eneo hatari karibu na lango Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1 .Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar aliyeilaza kimiani Mexico ilikuwa imeongoza hadi dakika ya 88 ya kipindi cha pili kabla Wesley Sneijder kuisawazishia Uholanzi kabla ya Huntelaar kufunga penalti iliyozua ubishi mkubwa.Herrera alisema kuwa haikufaa refarii kutoka ulaya alipewa mechi kati ya timu kutoka ulaya na Marekani ya kusini.Kwa sasa wapenzi wa soka duniani wanasubiri uamuzi wa FIFA kufuatia habari za Robben.


Said PiePie,Nairobi.

RAMBIRAMBI KWA SIMIYU


Strika wa Ulinzi Stars Anthony Mulinge Ndeto
            Naibu nahodha wa klabu ya Ulinzi Stars Anthony Mulinge Ndeto ametuma rambirambi zake kwa aliyekua strika wa Ulinzi Warriors Dan Mavious Simiyu.
Aidha Ndeto ameongeza kuwa Ulinzi imepoteza strika mahiri aliyejitolea kukuza mchezo wa soka katika klabu hicho.
Ndeto amewatakia jamaa familia na rafiki kuwa na subra wakati huu mgumu kwa kumpoteza mpendwa wao.Simuyu aliiaga dunia  Julai 24 wiki ilililopita baada ya kuvamiwa na majambazi alipokua akisafiri toka Nairobi kuelekea Nakuru.

Said PiePie,Nairobi.