Wednesday, 16 July 2014

LIVERPOOL YAMSAJILI MARKOVIC


Lazar Markovic aliyekua mchezaji wa Benfica
 Klabu ya  Liverpool imemsajili  Lazar Markovic  kwa kima cha Pauni millioni 20 kutoka Benfica.Mserbia huyo aliiwezesha klabu ya Benfica kutwaa taji la Ureno msimu uliopita na anasema anamatumaini makubwa ya kuwaridhisha mashabiki na mwenye club hiyo.Katika dirisha la usajili msimu huu Liverpool wamenasa wachezaji kadhaa wakiwemo Mshambuliaji Rickie Lambert, 32 kwa pauni £4m na Adam Lallana, mwenye umri wa miaka 26, kwa pauni £25m, wote walitokea Southampton na Divorc Origi kutokea humu nchini.

Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment