Thursday, 3 July 2014

ORIGI KUELEKEA UINGEREZA MSIMU UJAO



Divorc Origi,anayesakatia kabumbu Ubelgiji na Lille ya Ufaransa
      Mjombake Divorc Origi, Austin Oduor, amesema strika  huyo wa  taifa ya Ubelgiji anapania kuelekea Uingerza msimu ujao.Aidha Oduor, ameongeza kuwa strika yuko katika hali nzuri ya kuelekea Uingereza msimu ujao.Origi, mwenye umri wa miaka 19 ameonyesha mchezo mzuri kwenye mashindano ya kandanda ya kombe la dunia nchini Brazil, na kwa mara ya kwanza alicheza dakika zote tisini dhidi ya Marekani kwenye mechi yao ya raundi ya pili, na hatimaye Romelu Lukaku akaingia uwanjani naye Origi akapumzika.Miongoni mwa timu za ligi kuu ambazo zinammezea  Origi mate ni Liverpool, Tottenham Hotspurs na Arsenal lakini kuna dalili Liverpool itamnasa kinda huyo ambaye alizaliwa Ubelgiji wakati babake Mike Okoth, raia wa Kenya, alipokuwa akicheza kandanda ya kulipwa nchini humo.Origi mwenyewe anasema ana hamu sana ya kushiriki ligi kuu ya England bora apate klabu kitakachomfurahisha.Babake Origi ni shabiki sugu wa Liverpool hivyo basi huenda akamshawishi mwanawe ajiunge na bingwa hao mara 18 wa ligi kuu ya England.Lakini kabla mashindano ya kombe la dunia yaanze Okoth alisema atampa Origi uhuru wa kuamua ni klabu kipi anataka kuchezea England endapo atagura Lille ya Ufaransa.

Said PiePie,Nairobi