Friday, 20 June 2014

SSERENKUMA KUELEKEA DENMARK KWA MAJARIBIO


Dan Sserenkuma Strika wa Gor Mahia

         Strika wa Gor Mahia Dan Sserenkuma anapania kuelekea nchini Denmark kwa majaribio ya kujiubnga na klabu ya daraja la kwanza ya  HB Koge.Sserenkuma ataelekea Denmark tarehe 28 mwezi huu na atarudi nchini tarehe 10  Julai. HB Koge pia inawachezaji wengine kutoka humu nchini kama vile Thobias Ndungu aliyekua mchezaji wa Harambee Stars na Emmanuel Ake.

Said PiePie,Nairobi

GOR KUMSAJILI SSENTAGO







Robert  Ssentago anayepania kuhamia Gor
   Strika wa Uganda Cranes  Robert Ssentogo anapania kujiunga na Gor Mahia FC. Kulingana na habari zilizotolewa na Naibu katibu wa Gor Mahia Ronald Ngala.Hapo awali Ssentogo alichezea URA ya Uganda na St Georges kule nchini Ethiopia

Said PiePie,Nairobi.

MECHI ZA INGWE ZAHAIRISHWA


 
 
Kikosi  cha Leopards almaarufu  Ingwe

    Mechi kati ya AFC Leopards na Western Stima iliyokuwa imeratibiwa kukaragazwa Jumapili ya Juni 22 na mechi nyingine kati yao na Bandari ambayo iliratibiwa kusakatwa Jumatano ya Juni 25 zimehairishwa hii ni kuilingana na ripoti iliyotolewa mapema hii leo shirikisho la ligi ya primia humu nchini KPL

Huku hayo yakijiri Top Fry watakua wenyeji  wanamvinyo Tusker FC watakapo menyana mnamo Jumatano ya Juni 25 katika uchanjaa wa Afraha mjini Nakuru.

Said PiePie,Nairobi.


UINGEREZA YAZIDI KUDIDIMIA



Edinson Cavani anayesakatia Uruguay na Paris Saint-Germain
         Katika dimba la Kombe la Dunia, Uingereza wanashikilia mkia kwa kundi lao baada ya kuzamishwa na Uruguay kwa kufungwa 2-1. Luis Suarez ndiye aliyeiangamiza Uingereza kwa kuyafunga magoli yote mawili wakati Wayne Roney akiifungia Uingereza goli la kufutia machozi na ambalo ndilo lake la kwanza katika Kombe la Dunia. Kwingineko, Colombia wamefuzu katika awamu ya 16 baada ya kuwabwaga Cote d'Ivoire magoli mawili kwa moja. Katika mchuano mwingine, Japan na Ugiriki zilitoka sare ya kutofungana bao katika. Ugiriki ililazimika kucheza kwa dakika 52 bila ya nahodha wake Kostas Katsouranis, ambaye alitimuliwa uwanjani kwa kufanya makosa yaliyompa kadi mbili za njano. Hii leo Ijumaa, Italia watashuka dimbani dhidi ya Costa Rica wakati Uswisi wakikabana koo na Ufaransa kabla ya Honduras kuangushana na Equador.

Said PiePie,Nairobi.