Tuesday, 15 July 2014

VIJANA WA TRANZOIA WAREJEA KUTOKA BRAZIL

   
Baadhi ya vijana wanao sakatia Trans Nzoia Youth Sports Association,

  Timu nchini wa umri usiozidi  miaka 18 ya Trans Nzoia Youth Sports Association,, kutoka nchini Kenya wamerejea nyumbani baada ya kushiriki kwenye mashindano ya wachezaji watano kila upande ya Football For Hope Festival mjini Rio De Janeiro, Brazil.Timu ya Delta Culture ya Cape Verde ilishinda mashindano hayo kwa kuilaza Sport Dans La Ville ya Ufaransa bao 1-0 mechi ya fainali.Timu  ya Cape Verde na Tysa ni baadhi ya timu nane za Afrika zilizoshiriki mashindano hayo yaliyojumuisha timu kutoka mataifa 32.Wachezaji hao, walitizama mechi ya robo-fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa wanasema mbali na kandanda, wamejifunza mengi kuhusu maadili mema.Timu hiyo ilimaliza mechi zake zote bila kupoteza.

Said PiePie,Nairobi.

STARS KUMENYANA NA BURUNDI LEO


Kikosi cha Stars katika kambi ya mafunzo
      Timu ya taifa ya harambee stars itachuana na Burundi katika mechi ya kirafiki hii katika uga wa Nyayo.Mechi ya leo ni katika maandalizi ya michuano ya  kufuzu  AFCON 2015 mechi itakayo karagazwa huku Lesotho katika uga wa Maseru Julai 20.
Katika mchuano wa leo refarii wa katikati ya uwanja ni Ssali Mashood akisaidiwa na Bugembe Hussein na   Ngobi Balikoowa wote kutokkea nchi ya Uganda.Mechi hiyo imeratibiwa kusakatwa hii leo saa kumi na moja jioni katika uga wa Nyayo

Said PiePie,Nairobi.