Friday, 20 June 2014

UINGEREZA YAZIDI KUDIDIMIA



Edinson Cavani anayesakatia Uruguay na Paris Saint-Germain
         Katika dimba la Kombe la Dunia, Uingereza wanashikilia mkia kwa kundi lao baada ya kuzamishwa na Uruguay kwa kufungwa 2-1. Luis Suarez ndiye aliyeiangamiza Uingereza kwa kuyafunga magoli yote mawili wakati Wayne Roney akiifungia Uingereza goli la kufutia machozi na ambalo ndilo lake la kwanza katika Kombe la Dunia. Kwingineko, Colombia wamefuzu katika awamu ya 16 baada ya kuwabwaga Cote d'Ivoire magoli mawili kwa moja. Katika mchuano mwingine, Japan na Ugiriki zilitoka sare ya kutofungana bao katika. Ugiriki ililazimika kucheza kwa dakika 52 bila ya nahodha wake Kostas Katsouranis, ambaye alitimuliwa uwanjani kwa kufanya makosa yaliyompa kadi mbili za njano. Hii leo Ijumaa, Italia watashuka dimbani dhidi ya Costa Rica wakati Uswisi wakikabana koo na Ufaransa kabla ya Honduras kuangushana na Equador.

Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment