|  | 
| Edinson Cavani anayesakatia Uruguay na Paris Saint-Germain | 
         Katika dimba la Kombe la Dunia, Uingereza wanashikilia mkia kwa kundi lao 
baada ya kuzamishwa na Uruguay kwa kufungwa 2-1. 
Luis Suarez ndiye aliyeiangamiza Uingereza kwa kuyafunga magoli yote mawili 
wakati Wayne Roney akiifungia Uingereza goli la kufutia machozi na ambalo 
ndilo lake la kwanza katika Kombe la Dunia. Kwingineko, Colombia wamefuzu 
katika awamu ya 16 baada ya kuwabwaga Cote d'Ivoire magoli mawili kwa 
moja. Katika mchuano mwingine, Japan na Ugiriki zilitoka sare ya 
kutofungana bao katika. Ugiriki ililazimika kucheza kwa dakika 52 bila ya 
nahodha wake Kostas Katsouranis, ambaye alitimuliwa uwanjani kwa kufanya 
makosa yaliyompa kadi mbili za njano. Hii leo Ijumaa, Italia watashuka 
dimbani dhidi ya Costa Rica wakati Uswisi wakikabana koo na Ufaransa kabla 
ya Honduras kuangushana na Equador.
Said PiePie,Nairobi. 
 
No comments:
Post a Comment