 |
Kikosi cha timu ya taifa ya Brazil alamaarufu Samba Boys |
Brazil na Colombia zitamenyana kwenye mchezo wa
robo fainali ya Kombe la Dunia hii leo mchuano huo utakaragaziwa Uwanjani Castelao mjini
Fortaleza.Mara ya mwisho Colombia kuilaza Brazil ilikuwa
mwaka 1991. Lakini, kipute hicho cha robo fainali ya Kombe la Dunia
kinaikuta Colombia ikiwa kwenye ubora mkubwa na kuundwa na nyota makini
akiwemo Rodriguez, Juan Cuadrado na Jackson Martinez na kuwafanya Brazil
kuwa kwenye presha kubwa sana.Cuadrado, ndiye mchezaji aliyepiga pasi nyingi
zilizozaa mabao kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia, akiwa amechangia
mabao manne kwa kikosi cha Colombia.Kwenye hatua ya 16 bora, Brazil ilipata shida
dhidi ya Chile na kufanikiwa kuwatupa nje kwa mikwaju ya penalti 3-2,
wakati Colombia iliichapa Uruguay kiulaini mabao 2-0, shukrani kwa mabao
hatari ya Rodriguez na kazi nzuri ya staa wa taifa hilo, Cuadrado.Utamu wa mchezo huo utazikutanisha timu mbili
zinazobebwa na mastaa vijana, Neymar kwa upande wa Brazil na Rodriguez
kwa Colombia. Kwenye fainali hizo, Neymar ametikisa nyavu mara mbili,
moja pungufu ya mpinzani wake wa leo, James Rodriguez.
 |
Radamel Falcao Strika wa Colombia |
Robo fainali hiyo itatanguliwa na ile kati ya
Ufaransa na Ujerumani itakayopigwa kwenye Uwanja wa Maracana jijini Rio
de Janeiro. Mechi hiyo ya Ufaransa na Ujerumani ni ya kihistoria.
Timu hizo mbili ziliwahi kumenyana kwenye hatua ya
nusu fainali ya Kombe la Dunia 1982, ambapo Wajerumani walishinda kwa
mikwaju ya penalti. Ufaransa itaingia kwenye mchezo huo ikitaka kulipa
kisasi, lakini jambo hilo litafanywa na wachezaji 21 kati ya 23 kwenye
kikosi hicho cha Les Bleus ambao walikuwa hawajazaliwa wakati timu yao
ikifungwa kwa penalti na Ujerumani katika fainali hizo.Kiungo Blaise Matuidi atabeba majukumu ya Ufaransa
kwenye sehemu ya kiungo sambamba na Paul Pogba na Yohan Cabaye, ambao
watakuwa kwenye vita ya nguvu dhidi ya Toni Kroos, ambaye amefunika kwa
kupiga pasi katika fainali hizo za Brazil.Aidha mechi nyingine za hatua ya robo fainali
zitaendelea kesho,ambapo Argentina itakajimwaya uwanjani na Ubelgiji
na Uholanzi itakapokwaruzana na Costa Rica.
Said PiePie,Nairobi