![]() |
David Luiz ashangaa baada ya kulazwa na Ujerumani |
Mchecheto wa timu ya Brazil kunyakua Kombe la
Dunia mwaka huu ulizimwa hapo jana baada ya Ujerumani kuwarindima mabao 7-1 katika uwanja wa Estadio Mineirao ulioko Belo Horizonte.
Hicho ndicho kilikuwa kichapo
kikubwa kuwahi kutokea katika historia yao ya miaka 100 ya soka.
Kocha Luiz Felipe Scolari
aliyeonekana kupatwa na mshangao mkubwa,amewaomba mashabiki wamsamehe kutokana na makosa waliyofanya. Rais Dilma
Roussef pia alituma ujumbe wa kuituliza mioyo ya mashabiki.Thomas Müller ambaye alifunga goli
lake la tano katika dimba hili, alisema hawakuamini matokeo hayo ya kushangaza. Tikiti ya Ujerumani kuelekea mjini Rio ilipatikana baada ya kipindi cha kwanza
cha maangamizi ambacho walifunga magoli manne katika dakika sita.
Thomas Müller alifungua ukurasa wa mabao
katika dakika ya 11 kutokana na mkwaju wa kona. Miroslav Klose kisha akatia
kimyani la pili katika dakika ya 23 ambalo lilikuwa lake la 16 na kumfanya
kuwa mfungaji wa magoli mengi katika historia ya Kombe la Dunia.
![]() |
Kilio cha mashabiki wa timu ya Brazil hakikuzulika |
Mashabiki wa Brazil hawakuamini
macho yao namna timu yao ilivyokalifishwa uwanjani kutoka mwanzo.Toni Kroos alifunga
katika dakika ya 24 na 26 mtawalia ili kufanya mambo kuwa 4-0 na kisha Sami Khedira
akabusu wavu na kufikisha 5-0 katika dakika ya 29.Goli la dakika ya mwisho lake Oscar
la kufutia machozi hata halikuwatikisa mashabiki wa Brazil ndani ya uwanja.
Kocha wa Ujerumani Joachim Löw amesema Brazil walishtuka baada ya kufunwga
magoli ya mapema, kwa sababu hawakutarajia hilo. Hawakujua wafanye nini. Safu
yao ya ulinzi haikuwa imejipanga. Ujerumani sasa wanajiandaa kwa fainali
itakayochezwa katika uwanja wa Maracana Jumapili tarehe 13. Na mpinzani wao
atajulikana hiii leo, kati ya Argentina na Uholanzi ambao wanakutana katika nusu
fainali ya pili.
Said PiePie,Nairobi.