Saturday, 12 July 2014

GOR YAZIMA STIMA


Kikosi cha Gor kwenye mbwembwe
     Gor Mahia imeandikisha ushindi mnono hii leo baada ya kuwalaza Western Stima  2-0 katika mchuano wa ligi ya primia nchini ulio karagaziwa katika uga wa Afraha mjini Naivasha jioni ya leo. Eric Ochieng aliyekuwa mchezaji wa  Talanta FC hapo awali na Timothy Otieno waliwatia Kogalo kifua mbele kwa kufunga mabao mawili mtawalia.Gor walimiliki mpira kwa mda mrefu katika dakika za kwanza hata hivyo katika dakika ya nane Stima walivamia lango la Gor huku wakiponea kwenye tundu la sindano.
Baadhi ya wachezaji wa Western Stima
Bao la kwanza la Gor lilipatikana katika dakika ya 61 kupitia kona iliyocharazwa na   Erick Ochieng.Huku bao la pili likitiwa kimiani naTimothy Otieno.












  Aidha kocha wa Gor,Bobby Williamson amewapongeza vijana wake kwa kuonyesha mchezo mzuri uliokomaa.Refarii wa katikati ya uwanja alikua  Amos Ichingwa.Wakati uo huo Sony sugar iewalaza Tusker Fc 1-0


Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment