 |
Uga wa Corithians Sao Paulo unachukua mashabiki 61,500 |
Sherehe za Ufunguzi wa Kombe la
Dunia Brazil 2014 ziliaanza kwa mbwembwe
ya aina yake huku mwimbaji wa kimataifa
Jinnifer Lopez akipamba jukwaa Katika uga wa Corithians Sao Paolo.Timu ya taifa la Croatia
iliwachezesha : Pletikosa; Srna, Ćorluka, Lovren, Vrsaljko; Modrić, Rakitić,
Perišić, Brozović; Olić, Jelavić huku nao wapinzani wao Brazil wakiwashirikisha
katika kikosi chao : Cesar; D.Alves, T.Silva, D.Luiz, Marcelo; Paulinho,
L.Gustavo; Hulk, Oscar, Neymar; Fred.
 |
Marcelo Vieira anayeichezea Real
Madrid |
Mercelo alijifunga katika kipindi cah
kwanza na kuipa Croatia bao la kwanza .
Neymar aliifungia bao la kwanza na pili Brazil
kupitia kwa mkwaju wa penalti hata hivo maswali yanazidi kuibuka kuhusiana na penalti hiyo.Mchezaji huyo aliiandikisha
rekodi kwa kuwa mchezaji wa kwanza kuonyeshwa kadi ya Njano kwa kumpiga kumbo Modric
katika mechi za kombe la dunia mwaka huu.Katika dakika ya 47 Neymar alifanyiwa badiliko huku mchezaji Ramires
anayeisakatia Chelsea akijaza pengo lake.Oscar amhakikishia kocha Luiz Felipe
Scolari ushindi muhimu katika mechi ya ufunguzi wa dhidi ya Croatia kwa
kupachika kimiani bao la tatu na la ushindi.
Kocha wa Croatia Niko Kovac ambaye
alikuwa na hasira amesema mwamuzi kutoka Japan Yuichi Nishimura aliyesimamia
pambano hilo la jana alikuwa hayuko katika kiwango chake, baada ya kutoa
penalti kwa Brazil ambayo imebishaniwa na kubadilisha kabisa mwelekeo wa mchezo
huo wa ufunguzi.
Croatia wako katika nafasi ya 18 ya
orodha ya FIFA ya timu bora duniani , ilikuwa ikijaribu kuzuwia na kuwatuliza
Brazil katika kipindi cha pili hadi pale refa Yuichi Nishimura alipoamua upigwe
mkwaju wa penalti baada ya mshambuliaji wa Brazil Fred kuanguka wakati
akipambana na mlinzi wa Croatia Dejean Lovren
Hii leo Simba
wa Nyika , Cameroon , wataingia uwanjani kupambana na Mexico katika mchezo
mwingine wa kundi A, wakati mabingwa watetezi Uhispania inaanza kampeni ya
kurelijesha taji hilo mjini Madrid kwa kupambana na Uholanzi katika mchezo wa
kundi B.
Said PiePie,Nairobi.