Monday, 7 July 2014

KOCHA WA ALGERIA AFUNGANYA VIRAGO


Aliyekua kocha wa timu ya taifa ya Algeria Vahid Halilhodzic
    Timu ya taifa ya  algeria imepatwa na pigo baadaya kocha wake kuijuzulu,Vahid Halilhodzic amejiuzulu licha ya ombi la kibinafsi kutoka kwa rais Abdelaziz Bouteflika akimsihi asijiuzulu.Vahid amekuwa Kocha wa Desert Folks kwa miaka mitatu.Vahid ni mzaliwa wa nchi ya Bosnia alielekeza timu hiyo katika michuano mbalimbali. Timu yake ilikuwa imesalia kati ya timu zingine 16 bora katika kitengo hicho cha ligi ya kombe la dunia.Timu ya Algeria baada ya kuilaza South Korea mabao manne kwa mawili, haikuponea mchujo baada ya kulazwa mabao mawili kwa moja dhidi ya timu ya Ujerumani.
Aidha vijana wa Vahid  walilazwa 2-1 dhidi ya Belgium, na kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Urusi na kufuzu kwenda raundi ya pili.


Said Piepie,Nairobi

LIVERPOOL YAMNASA ORIGI




Divock Origi anayepania kuelekea Liverpool msimu ujao
     Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amesema klabu yake  imekubaliana ya Lille ya Ufaransa kumsajili mshambulizi wa Ubeljiji mzaliwa wa Kenya Divock Origi kwa kima  cha pauni milioni £10m.Wakati uo huo Liverpool  inapania kumsajili kiungo cha kati wa Serbia na Benfica Lazar Markovic kwa kima cha pauni milioni £25m.Origi hata hivyo anatarajiwa kukamilisha mazungumzo juma lijalo .Aidha  Liverpool inatarajia kumuuza  Luis Suarez, kwa kwa klabu ya Barcelona kwa pauni milioni £75m.Barca imeonesha niya ya kumnunua Suarez fauka ya matatizo yaliyokumba baada ya kumngata mlinzi wa Italia Chiellini katika mechi ya kombe la dunia.Liverpool vilevile inamtaka Alexis Sanchez, katika uhamisho huo wa Suarez .Liverpool tayari imewanunua Rickie Lambert,32, kiungo Adam Lallana ,kutoka Southampton kwa gharama ya pauni ya milioni £29m.Kwa sasa Rodgers anatafuta kuimarisha kikosi chake kabla ya kushiriki mchuano wa kuwania ubingwa wa bara uropa mwakani baada ya kumaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya Man City.


Said PiePie,Nairobi