Thursday, 17 July 2014

DEMBA BA AELEKEA UTURUKI


Aliyekua Strika wa Chelsea Demba Ba


  Aliyekua Strika wa Chelsea Demba Ba amewasili Uturuki anakotarajiwa kukamilisha uhamiaji wake kutoka Chelsea hadi Besiktas kwa gharama ya £8m. Strika huyo mwenye umri wa mika 29 ameyathibitisha hayo katika mtandao wa Twitter akiwaamevalia  jezi ya Besi-ktas.Aidha.Wakati uo huo Chelsea wamejibu kwa kumshawishi Filipe Luis aihame Atletico Madrid ili ajiunge nao.Msimu uliopita Luis alishiriki mechi zaidi ya 40 na kilele ikawa Atletico kushinda La Liga kwa mara ya kwanza tangu 1996.Demba Ba amewahi kuifungia Chelsea mabao 14.

Said PiePie,Nairobi.

ARSENALI YAPANIA KUMNASA KHEDIRA


Sami Khedira aliyekua kiungo wa Real Madrid

    Klabu ya Arsenali imefikia hatua ya kumsajili kiungo wa kati  Sami Khedira.tokea Real Madrid kwa kima cha £20m.Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 ni mzawa wa Tunisia laikini kwa sasa anasakata soka ya kulipwa nchini Ujerumani kandarasi yake bado ipo kule  Santiago hadi mwaka wa 2015.Maelewana na klabu ya Arsenali wanazidi kunoga,aidha wanabunduki wamesha wasajili mhispania Alexis Sanchez ambaye hapo awali alikua akiwasakatia Barcelona.


 Said PiePie,Nairobi.

DIEGO AELEKEA CHELSEA


Diego Costa aliyekua strika wa  Atletico Madrid,
Strika wa Atletico Madrid,Diego Costa amejiunga na klabu ya Chelsea kwa kwa kandarasi ya miaka mitano kwa kima cha  £32mAidha mshambulizi huyo amekuwa mchezaji wa tatu kujiunga na Chelsea baada ya Cesc Fabregas na Mario Pasalic.Costa amefungia Atletico mabao 52  msimu uliopita ambapo walishinda taji la kwanza la La Liga tangu 1996 na kufikia kuwa mabingwa wa ligi.Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho aliongeza mshambulizi matata katika kipindi hicho.Costa atajiunga na mchezaji mwenza wa kimataifa Cesc Fabregas kutokana na matokeo duni ya uhispania katika kombe la dunia ambapo walibanduliwa nje katika hatua ya kwanza ya kikundi.Wakati uo huo Costa ameonyesha furaha yake kujiunga na Chelsea akisema kuwa ataonyesha umahiri wake ulaya.

Said PiePie,Nairobi.