Monday, 30 June 2014

INGWE HAIKOPESHI KWA SASA.



Kikosi cha Leopards alamaarufu Ingwe

             Timu ya AFC Leopards imefutilia mbali uhamisho wa wachezaji wake iliokuwa imepania kuwasajili kwa mkopo,miongoni mwa wachezaji hao ni pamoja na Strika Dennis Dodi, Duncan Otieno na Sadiq Mohammed.Kulingana na katibu wa Ingwe Timothy Lilumbi amesema kuwa maelewano na klabu mbalimbali hayajaafikiwa.Leopards ilikua inapania kusajili wachezaji katika klabu ya Kakamega Homeboyz, Thika United na Mathare United.


Said PiePie,Nairobi.

PODOSKI KUKOSA MECHI DHIDI YA ALJERIA



Lukas Podolski Strika wa Ujerumani
     Lukas Podolski hatashiriki  mchuano wa kufuzu katika robo fainali dhidi ya Algeria utakaochezwa hii leo.Kocha wa Ujerumani Joachim Löw amewadokezea waandishi habari katika kambi ya mafunzo ya Ujerumani ya Santo Andre kuwa Podolski hatakuwa tayari kwa wakati unaofaa kucheza mpambano wa Algeria, akisema kuwa mchezaji huyo wa pembeni wa Arsenal atastahili kupumzika kwa siku mbili au tatu.Beki Jerome Boateng amepata jeraha jingine, mara hii akiumia katika goti lake la kushoto. Löw amesema jeraha hilo siyo ba ya sana.Dhidi ya Algeria, Ujerumani inapambana na timu dhabiti zaidi ya Afrika katika dimba hilo kufikia sasa. Löw amesema Desert Warriors ni hatari mno na wenye nguvu uwanjani na hivyo haitakuwa kazi rahisi kwa vijana wake, hata hivyo  ameongeza kuwa timu yake inaweza kuimarika baada ya kutoka sare na Ghana na kuwapiku kwa ushindi mdogo sana timu ya Marekani yake Jürgen Klinsmann katika hatua ya makundi.

Said PiePie,Nairobi


"SIKUANGUSHWA" ROBBEN AKIRI.


Strika wa Uholanzi Arjen Robben katika mechi dhidi ya Mexico
                    Strika wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa hakutegwa bali alijiangusha tukio lilisababisha tim uyake kutuzwa penaltiWakati uo huo kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .Robben alikunguwa katika eneo hatari karibu na lango Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1 .Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar aliyeilaza kimiani Mexico ilikuwa imeongoza hadi dakika ya 88 ya kipindi cha pili kabla Wesley Sneijder kuisawazishia Uholanzi kabla ya Huntelaar kufunga penalti iliyozua ubishi mkubwa.Herrera alisema kuwa haikufaa refarii kutoka ulaya alipewa mechi kati ya timu kutoka ulaya na Marekani ya kusini.Kwa sasa wapenzi wa soka duniani wanasubiri uamuzi wa FIFA kufuatia habari za Robben.


Said PiePie,Nairobi.

RAMBIRAMBI KWA SIMIYU


Strika wa Ulinzi Stars Anthony Mulinge Ndeto
            Naibu nahodha wa klabu ya Ulinzi Stars Anthony Mulinge Ndeto ametuma rambirambi zake kwa aliyekua strika wa Ulinzi Warriors Dan Mavious Simiyu.
Aidha Ndeto ameongeza kuwa Ulinzi imepoteza strika mahiri aliyejitolea kukuza mchezo wa soka katika klabu hicho.
Ndeto amewatakia jamaa familia na rafiki kuwa na subra wakati huu mgumu kwa kumpoteza mpendwa wao.Simuyu aliiaga dunia  Julai 24 wiki ilililopita baada ya kuvamiwa na majambazi alipokua akisafiri toka Nairobi kuelekea Nakuru.

Said PiePie,Nairobi.

Friday, 27 June 2014

ALGERIA NDANI YA 16 BORA





Mashabiki hakiki wa timu ya taifa ya Algeria almaarufu Desert folks
       Mashabiki wa timu ya taifa ya  Algeria waliandaa serehe babubkubwa baada ya timu yao kufuzu kwa michuano ya mchujo ya kombe la dunia kwa mara ya kwanza.Algeria ilifuzu katika awamu hiyo ya pili nchini Brazil baada ya kupata sara ya bao moja kwa moja na Urusi ambao waliobanduliwa katika michuano hiyo.Fataki ziliwashwa usiku kucha katika mji mkuu wa Algeria, Algiers huku makundi ya raia wakicheza densi na kupeperusha bendera.
Misafara ya magari ilipitia katika maeneo mengi ya mji  mkuu Algiers huku barabara huku shangwe,nderemo na vifijo vikimiliki anga.Katika raundi ya pili, timu ya Algeria itakabana koo na Ujerumani siku ya jumatatu.Katika michuano ya kombe la dunia mnamo mwaka 1982,Ujerumani ilishtumiwa kwa kucheza sare na Austria kimakusudi ili kuhakikisha kuwa timu zote mbili zinafuzu ili kuiondoa Algeria.


Said PiePie,Nairobi

Thursday, 26 June 2014

SUAREZ NJE MIEZI 4

Luiz Suarez strika wa Uruguay
    Luis Suarez amepigwa marufuku ya mechi tisa na shirikisho FIFA baada ya kupatikana na kosa la kumng'ta Giorgio Chiellini kwenye mechi yao ya kombe la dunia nchni Brazil.Suarez pia  hatajihusisha na shughuli za kandanda kwa miezi minne na kutozwa faini ya dola elfu mia moja.Kutokana na adhabu hiyo Suarez sasa hatashiriki tena kwenye mechi zilizosalia za kombe la dunia.Kutokana na adhabu hiyo iliyochukuliwa na kamati ya nidhamu ya Fifa Suarez sasa hatashiriki kwenye mechi ya raundi ya pili kati ya Uruguay na Columbia Juni tarehe 28.
Adhabu hiyo pia inamaanisha Suarez hatashiriki kwenye mechi za Uruguay zijazo za kombe la dunia endapo timu itazidi kusonga mbele na zile zijazo za kufuzu kwa mashindano ya kombe la dunia.
Kamati hiyo ya nidhamu ya Fifa imesema Suarez hatakiwi kuingia kwenye uwanja wowote Uruguay inapocheza wakati wa adhabu hiyo ya kutocheza mechi tisa za kimataifa.Ripoti hii imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya Fifa Claudio Sulser .Aidha Kamati ya Fifa imetilia maanani kila kitu kwenye kitendo hicho kabla ya uamuzi huo.Mashabiki wengi duniani wamemshutumu vikali Suarez kwa kumng'ata mchezaji huyo wa Italia kwani hii ni mara ya tatu anapatikana na hatia hiyo.

Said PiePie,Nairobi.

UFARANZA KUKUTANA NA NIGERIA MKONDO WA PILI



Kikosi cha timu ya Ufarnza
         Ufaranza ilikamilisha mechi za makundi kwa sare tasa dhidi ya Ecuador.Kwa sasa Ufaransa imesalia kileleni mwa kundi E ikiwa na alama 7 moja zaidi ya Switzerland iliyoisakama Iran katika mechi ya mwisho.Nao Argentina  walifuzu katika raundi ya 16 bora ambapo sasa watachuana na Nigeria .Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Mechi hiyo ilishuhudia kadi nyekundu ya nane katika mashindano haya ya kombe la dunia ,nahodha wa Ecuador Antonio Valencia alipofurushwa uwanjani baada ya kumchezea vibaya Lucas Digne.Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Ufaransa sasa itamenyana  na Nigeria waliomaliza mechi yao ya kundi F kwa kushindwa na Argentina kwa mabao 3-2 siku ya Jumatatu tarehe 30 katika Estadio Di Nationale.Washindi wa kundi hilo Argentina watakuwa na kibarua kigumu dhidi ya Switzerland Jumanne ijayo katika uga wa Arena De Sao Paulo.


 Said PiePie,Nairobi.