Monday, 30 June 2014

"SIKUANGUSHWA" ROBBEN AKIRI.


Strika wa Uholanzi Arjen Robben katika mechi dhidi ya Mexico
                    Strika wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa hakutegwa bali alijiangusha tukio lilisababisha tim uyake kutuzwa penaltiWakati uo huo kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .Robben alikunguwa katika eneo hatari karibu na lango Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1 .Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar aliyeilaza kimiani Mexico ilikuwa imeongoza hadi dakika ya 88 ya kipindi cha pili kabla Wesley Sneijder kuisawazishia Uholanzi kabla ya Huntelaar kufunga penalti iliyozua ubishi mkubwa.Herrera alisema kuwa haikufaa refarii kutoka ulaya alipewa mechi kati ya timu kutoka ulaya na Marekani ya kusini.Kwa sasa wapenzi wa soka duniani wanasubiri uamuzi wa FIFA kufuatia habari za Robben.


Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment