Thursday, 26 June 2014

SUAREZ NJE MIEZI 4

Luiz Suarez strika wa Uruguay
    Luis Suarez amepigwa marufuku ya mechi tisa na shirikisho FIFA baada ya kupatikana na kosa la kumng'ta Giorgio Chiellini kwenye mechi yao ya kombe la dunia nchni Brazil.Suarez pia  hatajihusisha na shughuli za kandanda kwa miezi minne na kutozwa faini ya dola elfu mia moja.Kutokana na adhabu hiyo Suarez sasa hatashiriki tena kwenye mechi zilizosalia za kombe la dunia.Kutokana na adhabu hiyo iliyochukuliwa na kamati ya nidhamu ya Fifa Suarez sasa hatashiriki kwenye mechi ya raundi ya pili kati ya Uruguay na Columbia Juni tarehe 28.
Adhabu hiyo pia inamaanisha Suarez hatashiriki kwenye mechi za Uruguay zijazo za kombe la dunia endapo timu itazidi kusonga mbele na zile zijazo za kufuzu kwa mashindano ya kombe la dunia.
Kamati hiyo ya nidhamu ya Fifa imesema Suarez hatakiwi kuingia kwenye uwanja wowote Uruguay inapocheza wakati wa adhabu hiyo ya kutocheza mechi tisa za kimataifa.Ripoti hii imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya Fifa Claudio Sulser .Aidha Kamati ya Fifa imetilia maanani kila kitu kwenye kitendo hicho kabla ya uamuzi huo.Mashabiki wengi duniani wamemshutumu vikali Suarez kwa kumng'ata mchezaji huyo wa Italia kwani hii ni mara ya tatu anapatikana na hatia hiyo.

Said PiePie,Nairobi.

UFARANZA KUKUTANA NA NIGERIA MKONDO WA PILI



Kikosi cha timu ya Ufarnza
         Ufaranza ilikamilisha mechi za makundi kwa sare tasa dhidi ya Ecuador.Kwa sasa Ufaransa imesalia kileleni mwa kundi E ikiwa na alama 7 moja zaidi ya Switzerland iliyoisakama Iran katika mechi ya mwisho.Nao Argentina  walifuzu katika raundi ya 16 bora ambapo sasa watachuana na Nigeria .Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Mechi hiyo ilishuhudia kadi nyekundu ya nane katika mashindano haya ya kombe la dunia ,nahodha wa Ecuador Antonio Valencia alipofurushwa uwanjani baada ya kumchezea vibaya Lucas Digne.Ufaransa itachuana na Nigeria katika mkondo wa pili wa kombe la dunia.Ufaransa sasa itamenyana  na Nigeria waliomaliza mechi yao ya kundi F kwa kushindwa na Argentina kwa mabao 3-2 siku ya Jumatatu tarehe 30 katika Estadio Di Nationale.Washindi wa kundi hilo Argentina watakuwa na kibarua kigumu dhidi ya Switzerland Jumanne ijayo katika uga wa Arena De Sao Paulo.


 Said PiePie,Nairobi.

FIFA YAMPIGA MARUFUKU BECKNERBAUER



 
Aliyekua Kocha wa Ujerumani Franz Beckenbauer

           Franz Beckenbauer amepigwa marufuku ya siku 90 kujihusisha na soka kwa kushindwa kutoa ushikiano wake kwa kamati ya uchunguzi ya FIFA.
Aidha FIFA imedokeza kuwa Beckenbauer alikua katika  kamati kuu ya Shirikisho la Kimataifa la soka (FIFA) ambalo mwaka 2010 li iliwapatia Qatar kuandaa michuano ya michuano  ya Kombe la Dunia kwa mwaka 2022,aliombwa mara kadhaa kutoa maelezo yake kuhusu uamuzi huo tata.Marufuku hiyo imewekwa kufuatia ombi la mwanasheria wa Marekani Michael Garcia mkuu wa jopo la uchunguzi wa kamati ya maadili ya FIFA ambaye anaongoza uchunguzi kuhusu uamuzi huo wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022.
         Jumatano Garcia aliuambia mkutano mkuu wa FIFA wa kila mwaka mjini Sau Paulo Brazil kwamba yeye na kamati yake tayari walikuwa na sehemu kubwa ya mamilioni ya nyaraka ambazo zimetajwa na gazeti la Sunday Times la Uingereza katika repoti ya karibuni inayodai kutolewa kwa rushwa katika harakati za kufanikisha Qatar ipate nafasi ya kuandaa michuano hiyo ya soka Kombe la Dunia.
Gazeti la Sunday Times limesema baadhi ya mamilioni ya nyaraka imeziona kuwa zinahusiana na malipo yaliyotolewa na mjumbe wa zamani wa kamati kuu ya FIFA Bin Hammam kwa maafisa ikiwa kama sehemu ya kampeni ya kuungwa mkono kwa harakati za Qatar kuandaa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
Kesi hiyo hivi sasa iko kwenye taratibu rasmi za uchunguzi chini ya mjumbe wa jopo hilo Vanessa Allard akiwa kama mkuu wa uchunguzi.Repoti rasmi ya uchunguzi huo inatarajiwa kutolewa hapo mwezi wa Julai.

Said PiePie,Nairobi.

Wednesday, 25 June 2014

SUAREZ AMNG'ATA GIORGIO


 
Luiz Suarez aendeleza ukandamizaji
                   Strika wa  Uruguay Luis Suarez anakabiliwa na marufuku  itakayomlazimu kukosa mechi nyengine za michuano ya kombe la dunia iwapo atapatikana na hatia ya kumng'ata mchezaji wa Italy Giorgio Chiellini katika mechi ya hapo jana.

Shirikisho la soka duniani FIFA limeanzisha uchunguzi wa kumuadhibu mcheza huyo kufuatia ushindi wa moja kwa bila dhidi ya Italy.
Chiellini amedai kwamba Suarez alimng'ata bega lake licha ya Suarez kudai kuwa ni mchazaji huyo aliyemchezea vibaya.

Giorgio Chiellini aonyesha jeraha baada ya kung'atwa na Suarez
  

Suarez mwenye umri wa miaka 27 huenda akapigwa marufuku ya kutoshiriki katika mechi 24 ama miaka miwili.
Refa aliyesimamia mechi hiyo kutoka Mexico Marco Rodriguez hakuchukua hatua yoyote kufuatia kisa hicho,lakini FIFA bado inaweza kumuadhibu Suarez.
Aliyekuwa mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya Liverpool Jan Molby anatarajia kwamba Suarez atapigwa marufuku kwa mechi zote za kombe hilo zilizosalia.



Said PiePie,Nairobi.

LAMOUCHI AGURA IVORY COAST



Aliyekua kocha wa Ivory Coast Sabri Lamouchi


        Kocha wa Ivory Coast Sabri Lamouchi amejiuzulu baada ya timu yake kuzabwa 2-1 na Ugiriki hapo jana katika mechi ya kuisismua
Lamouchi aliliambia jarida la AFP katika mahojiano jana baada ya mechi hiyo kumalizika aidha raia huyo wa Ufaranza mwenye umri wa mika 42 amesema kuwa kandarasi yake ilimalizika jana.
Hata hivyo amedokeza kuwa kushindwa kwake kulichangiwa na mchezo duni ambao wachezaji wake walionyeshwa baada ya kupoteza fursa tumbi nzima waliopata.Lamouchi ilianza kuwaongoza Ivory Coast mnamo Mei 2012.

Said PiePie,Nairobi.




MECHI ZA KPL ZAHAIRISHWA


                             

        Mechi saba za ligi ya primia humu nchini  zilizokuwa zimeratibiwa kusakatwa wikendi hii zihairishwa.Kulingana na afisa mkuu ya Ligi ya primia nchini Jack Oguda amesema kuwa hali hii imechangiwa na kusafiri kwa kikosi cha Harambee Stars  kuelekea Brazil
Aidha Oguda ameongeza kuwa michuano ya ligi ya primia itarejelewa kuanzia Jumamosi tarehe 5 Julai na Jumapili 6 mwezi ujao.


Said PiePie,Nairobi.