Tuesday, 17 June 2014

INGWE YAMTEMA MUSAJA

Hassan Mohamed ambaye ametemwa na Ingwe

     Strika  Hassan Mohammed almaarufu Musaja ametemwa na  AFC Leopards. Musaja hapo awali alichezea klabu ya  Kenya Revenue Authority (KRA) FC almetemwa kufuatia mchezo duni ambao alionyesha hapo awali
Habari hiz izimetolewa na Katibu wa mipango wa mipano Timothy Lilumbi wa klabu ya Ingwe.
Strika huyo alijiunga na Ingwe kwa kandarasi wa miak miwili kutoka KRA kwa kima cha shilingi alfu 200.


Said PiePie,Nairobi.

AGUERO ASEMA BADO YUPOYUPO MAN CITY




Sergio Aguero Strika wa Man City
    Mshambulizi matata wa timu ya Manchester City na  Argentina Sergio Aguero amepuzilia mbali madai kuwa anapani kuhamia klabu za Real Madrid na Barcelona.
Aguero aliyekua mchezaji wa  Atletico Madrid  hapo awali amezua uvumi mkubwa tangia ahamie Etihad 2011 kuwa ana miadi ya kurejea Uhispania.

Aguero alitoa tangazo rasmi katika  Radio Cadena Cope ya Uhispania pia alichapisha habari hizo katika jarida la The Citizens kuwa hana miadi yakugura Man City.
Aguero amefunga jumla ya mabao 28  mwaka 2013/2014 akiwa na Man City.


Said PiePie ,Nairobi

MAREKANI YAIZIMA GHANA




       John Brooks liliwapa Marekani ushindi uliotokana na kibarua kigumu wa magoli mawili kwa moja dhidi ya Ghana katika uwanja wa Estadio das Nunas mjini Natal
Clint Dempsey alifunga goli la kasi sana na ambalo ni la tano katika historia ya Kombe la Dunia, na kuwaweka kifua mbele vijana wa kocha Jurgen Klinsmann baada ya sekunde 29.
Andre Ayew aliwapa pointi 1 Ghana almaarufu Black Stars  alipofunga bao safi baada ya kuandaliwa pasi  kisigino na Asamoah Gyan, wakati kukiwa kumesalia dakika 8 katika kipindi cha kwanza
Uzembe wa Ghana ulimpa fursa beki wa Marekani Brooks kufunga kichwa safi kutokana na mkwaju wa kona zikiwa zimesalia dakika 5 mpira kumalizika. Hilo lilikuwa goli lake la kwanza la kimataifa, na likampa ushindi Jurgen Klinsmann ambaye ameadhimisha mchuano wa 50 akiwa na timu ya taifa ya Marekani.

        
Shabiki wa Ghana na mbwembwe zake
Black Stars walitawala mchezo kwa muda mrefu lakini mwishoni walijuta kwa kushindwa kuzitumia fursa zao  kufunga mabao.Marekani sasa itacheza mchuano ujao dhidi ya Ureno, ambao walizabwa magoli 4-0 na Ujerumani, wakiwa na matumaini kuwa wanaweza kufuzu katika 16 za mwisho.
Kocha Klinsmann amesema “kuna mambo ambayo tunaweza kuimarisha lakini leo tumepata points tatu tulizozihitaji sana”. Aliongeza kuwa “Ghana ni timu nzuri na wanajua namna ya kuumiliki mchezo. Hilo lilitarajiwa”.
Kocha wa Ghana Kwesi Appiah alikanusha madai kuwa mchezo wa vijana wake ulitokana na mgomo baridi wa wachezaji lakini akakiri kuwa Black Stars bado wasubiri malipo yao kamili ya marupurupu.
Ghana walifika katika robo fainali ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini mwaka wa 2010, sasa wanakabiliwa na mlima mkubwa wa kuukwea ili kujiondoa katika kundi hilo ambalo lina Ujerumani, Ureno.
Marekani imelipiza kisasi cha kushindwa katika michuano miwili ya kombe la dunia na Ghana .

Said Piepie,Nairobi.

Monday, 16 June 2014

GOR YAMSAINI OTIENO




       
 
Timothy Otieno Talanta Fc

     Klabu ya Gor mahia ametia mkataba wa miezi sita na kiungo wa kati  wa Talanta FC Timothy Otieno,Kiungo huyo anauwezo mkubwa na aliisaidia klabu yake hapo awali kunyakua mataji kadhaa hatua iliyopelekea klabu nyingi kummezea mate. Kiungo huyo.Alifuzu kutoka National Youth Talent Academy (NYTA) pia ni mwanafunzi wa zamani wa shule ya upili ya Kakamega.

Said PiePie,Nairobi.

GOAL TECHNOLOGY KUTUMIKA EPL MSIMU UJAO








         Klabu za ligi kuu ya soka nchini England zimeafikiana kutumia teknolojia ya camera katika maamuzi ya mchezo wa soka kuanzia msimu ujao.
Kampuni ya Uingereza ya Hawk-Eye imepewa mkataba wa kufunga vifaa maalumu kwenye viwanja vyote 20 vya timu za ligi kuu nchini England.
Hawk-Eye inajulikana kwa  teknolojia kama hiyo kwenye mchezo wa Tenesi na Kriketi,ambapo camera maalumu huweza kutambua iwapo mpira umegusa mstari ama la na kumjulisha mwamuzi na wasaidizi wake ndani ya sekunde chache.
Chama cha soka nchini England FA,kitafunga vifaa hivyo kwenye uwanja wa Wembley tayari kwa kutumika kwenye mchezo wa ngao ya jamii hapo mwezi wa nane mwaka huu.
Viwanja vya timu 17 zitakazosalia ligi kuu na zile 3 zitakazopanda daraja vitawekewa teknolojia hiyo na shughuli nzima itachukua wiki sita kukamilika.Msukumo wa kutumia teknolojia maalumu ya kutambua goli ilipata nguvu baada England kukataliwa goli lao la kusawazisha walipocheza na Ukraine,Mchezo ambao England walifungwa bao moja kwa bila kwenye michuano ya kombe la mataifa barani Ulaya mwaka 2012, Ambapo mwezi mmoja baadaye bodi ya vyama vya soka vya kimataifa (IFAB) katika kikao chake mjini Zurich kilipitisha teknolojia mbili ili zitumike kwenye michezo ya soka.Rais wa FIFA Sepp Blater amesema kukataliwa kwa goli la Frank Lampard kwenye mechi ya robo fainali kati ya England na Ujerumani mwaka 2010 katika michuano ya kombe la dunia,kulichangia kwa kiasi kikubwa maamuzi ya shirikisho hilo kupitisha sheria ya matumizi ya teknolojia ya kutambua goli.
Chama cha soka cha England kimesema teknolojia hiyo itaaanza kutumika msimu ujao.Kwa sasa Goal  Technology inatumika katika michuano ya kombe la dunia nchini Brazil.

Said PiePie,Nairobi.

TUSKER YAZIDI KUNOGA



Tusker  Fc washerehekea ushindi wao dhidi ya Ingwe
     Nahodha wa  Tusker Fc  almaarufu wanamvinyo Samwel Odhiambo amesema kuwa timu yake iko katika hali nzuri yaku kung’ang’ania taji la KPL msimu huu alisema haya mapema hii leo.Hapo jana Wanamvinyo hao ilicharaza Inmgwe mabao 2-1 katika mechi za Nane bora katika  uchanjaa wa Kinoru,Meru.Kwa sasa Tusker inashikilia nafasi ya tatu na alama 27 katika jedwali la ligi ya primia humu nchini.



Said PiePie,Nairobi.