Friday, 4 July 2014

"STARS HAISAFIRI KWA MATATU" ASEMA NYAMWEYA



Sam Nyamweya Mwenyekiti wa FKF

      Mwenyekiti wa shirikisho la kandanda nchini Sam Nyamweya anamtaka Gavana  wa Machakos Alfred Mutua aombe msamaha kwa matamshi aliyoyatoa kuwa timu ya taifa ya  Harambee Stars hutumia magari aina ya Matatu kwa usafiri wake hii ni kulingana na ripoti iliyochapishwa kwa mtandao wa shirikisho la FKF.Wakati uo huo Nyamweya alipinga madai hayo akisema kuwa Harambee Stars hutumia usafiri waa ndege.Huku hayo yakijiri Stars wanapania kumenyana na timu ya taifa ya Lesotho katika mchuano wa kufuzu katika mechi za AFCON 2015 Julai 19 Maseru Lesotho huku mchuano wa nyumbani ukiratibiwa kucharazwa Agosti 3 mjini Nakuru.


Said PiePie,Nairobi

No comments:

Post a Comment