![]() |
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Ujerumani kwenye kambi ya mazoezi |
Ujerumani na Argentina zitakutana kwenye
mechi ya fainali ya kombe la dunia Jumapili Julai tarehe 13 mjini Rio De
Janeiro.Aidha mshindi ataweka kibindoni dola
milioni 35 na wa pili $25 milioni, wa tatu $22milioni wa nne $20 milioni.Timu nne zilizoondolewa kwenye
robo-fainali zitapokea $14 milioni kila mmoja, timu nane zilizong'olewa raundi
ya pili $9 milioni na timu 16 zilizoondolewa raundi ya kwanza $8 milioni kila
mmoja.
![]() |
Mchezaji wa safu ya mbele wa Argentina Angel Di Maria |
Ujerumani ilifuzu kwa awamu ya fainali baada ya kuwalaza Brazil mabao 7-1 na
Argentina ikaiondoa Uholanzi mabao 4-2 kupitia mikwaju ya penalti ktika mechi
ya nusu-fainali. Kwa jumla timu 32 zimeshiriki mashindano ya mwaka huu kwenye
mechi 64 na wachezaji 736 wakajitosa uwanjani.Hii ni mara ya tatu Ujerumani na
Argentina wanakutana fainali ya kombe la dunia, mara ya kwanza ikiwa mwaka wa
1986 nchini Mexico Argentina ikashinda 3-2 kisha wakapatana tena mwaka wa 1990
nchini Italia na Ujerumani ikalipiza kisasi kwa kuinyoa Argentina bao 1-0.
Argentina ilifuzu baada ya kushinda
Uholanzi huku Ujerumani ikiwaadhibu Brazil 7-1.
Said PiePie,Nairobi.
No comments:
Post a Comment