Friday, 11 July 2014

KLOSE ATIA FORA NCHINI BRAZIL



 
Strika wa Ujeruamani Miroslav Klose
     Miroslav Klose wa  Ujeruamani ndiye mfungaji wa mabaoi mengi katika Kombe la Dunia, baada ya kufunga goli lake la 16 dhidi ya Brazil, na kuifuta rekodi ya mshambuliaji wa Brazil Ronaldo.Klose mwenye umri wa miaka 36, anacheza katika Kombe la Dunia kwa mara yake ya nne, tayari alikuwa ameifikia rekodi iliyowekwa na Ronaldo ya magoli 15 wakati alipofunga goli la kusawazisha katika mchuano waliotoka sare ya 2-2 dhidi ya Ghana katika awamu ya makundi kabla ya kufunga la 16 katika mechi ya nusu fainali dhidi ya Brazil mjini Belo Horinzonte.Goli hilo lilikuwa lake la kwanza katika nusu fainali ya Kombe la Dunia na mojawapo ya mabao muhimu kwa sababu liliiweka Ujerumani kifua mbele 2-0.Klose, mwanasoka mtulivu anayechezea klabu ya Lazio baada ya kuanzia Kaiserslautern, Wrder Bremen na Bayern Munich.Kocha wake Joachim Löw amemmiminia sifa mshambuliaji huyo, akisema kikosi kizima kimefurahishwa na mafanikio ya Klose, na ni mafanikio ambayo alistahili kuyapata.

Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment