|  | 
| Divock Origi anayepania kuelekea Liverpool msimu ujao | 
     Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amesema klabu yake  imekubaliana ya Lille ya Ufaransa kumsajili mshambulizi  wa Ubeljiji mzaliwa wa Kenya  Divock Origi kwa kima   cha pauni milioni  £10m.Wakati uo huo Liverpool  inapania kumsajili  kiungo cha kati wa  Serbia na Benfica  Lazar Markovic kwa kima cha pauni milioni  £25m.Origi hata hivyo anatarajiwa kukamilisha mazungumzo juma lijalo .Aidha  Liverpool inatarajia kumuuza   Luis Suarez, kwa  
kwa klabu ya Barcelona kwa pauni milioni  £75m.Barca imeonesha niya ya kumnunua Suarez fauka ya
 matatizo yaliyokumba baada ya kumngata mlinzi wa Italia Chiellini 
katika mechi ya kombe la dunia.Liverpool vilevile inamtaka  Alexis Sanchez, katika uhamisho huo wa Suarez .Liverpool  tayari imewanunua Rickie Lambert,32, kiungo Adam Lallana ,kutoka  Southampton kwa gharama ya pauni ya milioni £29m.Kwa sasa Rodgers anatafuta kuimarisha  
kikosi chake kabla ya kushiriki mchuano wa kuwania ubingwa wa bara uropa
 mwakani baada ya kumaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya 
Man City.
 
No comments:
Post a Comment