Monday, 7 July 2014

KOCHA WA ALGERIA AFUNGANYA VIRAGO


Aliyekua kocha wa timu ya taifa ya Algeria Vahid Halilhodzic
    Timu ya taifa ya  algeria imepatwa na pigo baadaya kocha wake kuijuzulu,Vahid Halilhodzic amejiuzulu licha ya ombi la kibinafsi kutoka kwa rais Abdelaziz Bouteflika akimsihi asijiuzulu.Vahid amekuwa Kocha wa Desert Folks kwa miaka mitatu.Vahid ni mzaliwa wa nchi ya Bosnia alielekeza timu hiyo katika michuano mbalimbali. Timu yake ilikuwa imesalia kati ya timu zingine 16 bora katika kitengo hicho cha ligi ya kombe la dunia.Timu ya Algeria baada ya kuilaza South Korea mabao manne kwa mawili, haikuponea mchujo baada ya kulazwa mabao mawili kwa moja dhidi ya timu ya Ujerumani.
Aidha vijana wa Vahid  walilazwa 2-1 dhidi ya Belgium, na kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Urusi na kufuzu kwenda raundi ya pili.


Said Piepie,Nairobi

No comments:

Post a Comment