![]() |
Timu ya AFC Leopards hapo jana ilinyakua ushindi baada ya kuwalaza kcb 3-0 katika mchuano wa timu nane bora katika mechi ya nusu fainali.Austin Ikenna ,Jacob Keli and Bernard Mang’oli waliisaidia Leopards kunyakua ushindi huo. Wanabenki KCB walionyesha mchezo mzuri katika kipindi cha kwanza hata hivyo walikumbwa na utasa wa mabao.KCB walifanya badiliko katika dakika za kwanza za 12 baada ya kiungo wao wa kati Hedson Mauda kujeruhiwa pengo lake lilijazwa na Ronald Musana aliyesajiliwa majuzi
Mabeki ya KCB walizembea mnamo dakika ya 40 nakumpa fursa Paul Were aliipenyeza pasi ya kimanjaro kwake Bernard Mangoli wingi wa kushoto naye hakusita ila alimpeleka madukani mlinda lango wa KCB Caleb Wafula huku akiiandikia Ingwe bao la pili
Kipindi cha pili kilianza na mabadiliko huku Joseph Shikokoti akitolewa nje na nafasi yake ikimilikiwa na Eric Masika.Kwa sasa ingwe imejikatia tiketi ya fainali itakapo kutana na wanamvinyo Tusker FC Juni 15.
Said PiePie, Nairobi
No comments:
Post a Comment