Tuesday, 1 July 2014

KOCHA WA NIGERIA AFUNGANYA VIRAGO



Aliyekua kocha wa Nigeria almaarufu Super Eagles  Stephen Keshi 
      Stephen Keshi  Kocha wa Nigeria amejiuzulu baada ya timu ya Super Eagles kuondolewa kutoka kwenye kipute cha kombe la dunia walipozabwa 2-0 na Ufaransa .Keshi mwenye umri wa miaka 52 alichukua wadhfa huo mwaka wa 2011 na akaiongoza timu hiyo na kutwaa ubingwa wa afrika mwaka uliopita .Wakati uo huo nahodha wa timu hiyo Joseph Yobo aliyejifunga bao la pili la Ufaransa naye pia ametangaza kustaafu .Keshi chini ya uongozi wake Super Eagles imefuzu kwa mara ya kwanza katika mkondo wa pili wa kombe la dunia tangu mwaka wa 1998 licha ya kukumbwa na migomo ya wachezaji wake wakidai malimbikizi ya marupurupu.kocha waliojiuzulu kufuatia matokeo duni katika kombe la dunia kutimia makocha 6.Hadi sasa kocha wengine waliojiuzilu ni pamoja na Luis Suarez, wa Honduras, Carlos Queiroz wa Iran's ,Alberto Zaccheroni wa Japan , Cesare Prandelli wa italia na Sabri Lamouchi wa Ivory Coast.Hapo awali Keshi, aliwahi kuhudumu kama kocha wa Mali na Togo.

Said PiePie,Nairobi.

No comments:

Post a Comment